Quantcast
Channel: MAFUNDISHO – Strictly Gospel
Viewing all articles
Browse latest Browse all 46

Roho ya Kukataliwa

$
0
0

kukataliiwa

Roho ya kukataliwa inawasumbua watu wengi. Wengi wanaosumbuka na kukataliwa inawezekana walikuwa na wazazi wasiojali, wazazi walitengana, wamelelewa na mzazi wa kambo, hawakuwa vizuri darasani, n.k. Kukataliwa kunaumiza sana na kunaua kabisa hali ya kujiamini na shetani huitumia sana kuharibu maisha ya watu. Shetani anawafanya watu wasahau kabisa juu ya upendo wa Mungu na kuendelea kuumia na kuteseka.

EFE. 3:19 “na kuujua upendo wake Kristo, upitao ufahamu kwa jinsi ulivyo mwingi, mpate kutimilika kwa utimilifu wote wa Mungu.”

Kukataliwa kunaleta vidonda kwenye hisia na visipotibiwa hukua na kuwa vidonda vya kiroho kama kutokusamehe, wivu, chuki, uchungu na kumlaumu Mungu. Vidonda hivi hufungua milango kwa roho chafu kukuingilia kupitia milango hiyo. Shetani anafurahia moyo wako ukijaa mawazo mabaya juu ya watu wengine unaowaona kwamba hawajakutendea mema.

Kukataliwa kunamfanya mtu kuwa na tabia zifuatazo:
1. Uasi
2. Unafiki (ukiwa mbele za watu fulani unabadilika ili ukubalike)
3. Kukataa wengine
4. Kila wakati kujihisi kuwa unakataliwa
5. Kuhitaji sana kukubaliwa na kila mtu
6. Kujihurumia
7. Kutokuwa tayari kukosolewa au kusahihishwa
8. Kutokuweza kupokea wala kuonyesha upendo.
9. Kumlaumu Mungu kwa hali uliyonayo
10. Kiburi
11. Ukiwa hata ukizungukwa na watu.
12. Kujiona huna thamani, wala tumaini
13. Wivu, chuki na husuda.

Wengine wanahisi kukataliwa wakati si kweli. Roho hii ya kukataliwa inakufanya uone kama kila ambaye hajafanya jambo fulani kukusaidia au kukufurahia basi anakukataa. Biblia inasema aonavyo nafsini mwake ndivyo alivyo. Pia kuna wanaojikataa wenyewe na kupelekea kujichukia. Hali hii hutokana na kushindwa kujisamee kwa kosa fulani ukilotenda siku za nyuma na likakuletea madhara makubwa.

Unapoweka thamani yako kwa wanadamu ni lazima utaona kukataliwa na kujikuta unaruhisu roho za kukataliwa kuingia kwako. Lazima utambue kuwa thamani yako inatoka kwa Mungu na si wanadamu wanakuonaje. Haijalishi nani anasema nini bali tafuta Mungu anasema nini. Acha kumlaumu Mungu na kujilaumu unayopitia, biblia imasema mapito ya mwenye haki ni mengi lakini Bwana humlinda na hayo yote.

Usiruhusu chuki, uchungu, hasira na wivu vipate nafasi ndani ya moyo wako. Soma neno la Mungu lijae ndani yako na maombi kwa wingi. Kataa roho ya kukataliwa isipate kibali ndani yako kwa kuondoa milango ambayo ni kutokusamehe, chuki, wivu, uchungu na kumlaumu Mungu. Usiangalie yule aliyekutendea mabaya na kukukataa kama vile yeye ndiye mwenye hatima ya maisha yako bali muangalie Mungu aliyeahidi kuwa nawe siku zote.

EBR. 13:5b-6
“kwa kuwa yeye mwenyewe amesema, Sitakupungukia kabisa, wala sitakuacha kabisa. Hata twathubutu kusema, Bwana ndiye anisaidiaye, sitaogopa; Mwanadamu atanitenda nini?”

Mambo ya kufanya kushinda kukataliwa
1. Mruhusu Roho mtakatifu akuonyeshe umeumizwa wapi na kwa kiasi gani kwa kukataliwa.
2. Samehe wale waliokuumiza
3. Tupilia mbali matunda ya kukataliwa: chuki, hasira, uasi, uchungu n.k.
4. Kubali kuwa Mungu amekukubali kupitia Yesu Kristo.
5. Jikubali

ZAB. 71:5-7, 13 
“Maana ndiwe taraja langu, Ee Bwana MUNGU, Tumaini langu tokea ujana wangu.    Nimekutegemea Wewe tangu kuzaliwa, Ndiwe uliyenitoa tumboni mwa mama yangu, Ninakusifu Wewe daima.    Nimekuwa kitu cha ajabu kwa watu wengi, Na Wewe ndiwe kimbilio langu la nguvu.    Waaibishwe, watoweshwe, adui za nafsi yangu. Wavikwe laumu na aibu wanaonitakia mabaya.”

Soma pia Ebrania 4:16 Zaburi 23 1 Samwel 53:4

–WomenofChrist Blog


Filed under: MAFUNDISHO

Viewing all articles
Browse latest Browse all 46

Trending Articles