Bwana asifiwe wapendwa
Nawasalimu nyote kwa Jina la Yesu Kristu.
Naombeni mkipata nafasi msikilize huyu mtumishi wa Mungu kutoka Uganda anaitwa John Mulinde
“After working in the power of the Holy Ghost and seeing signs, wonders and miracles, JOHN MULINDE was an Evangelist fully sure of his Salvation. But when JESUS revealed himself to him, he was shocked of what he was told.”
Mungu alimonyesha maisha yake ya ndani na kwa uhakika alimwambia kuwa kama angerudi wakati ule anauhakika angebaki.
Sikiliza mtu wa Mungu na Bwana atusaidie. tumuombe atupatie Roho ya Toba na tumuangalie yeye katika maisha yetu. tumuombe atufunulie siri za Neno lake ili tumjue yeye aliyetupenda hata akamtoa Mwanae Yesu ili aturudishe kwake
Kama Daudi alisema ‘funua macho yangu nione uzuri wa maneno yako’
Utakatifu ndo tunatakiwa kukimbizana nao maana bila huo hatutaweza kumuona Bwana. na hatutaweza kwa nguvu zetu wenyewe ndo maana Yesu akatuahidi Roho wa Mungu ili akae ndani yetu na atuongoze.
Naomba nisiseme sana, niwaache msikilize halafu basi mtaleta maoni yenu tuweze kujengana.
Kama ukishindwa kufungua hiyo link basi nenda youtube na u-type
shocking message from Jesus to John Mulinde. imepandikwa na Yves YN Nahishakiye
Mubarikiwe wapendwa.
-CM
Filed under: MAFUNDISHO
