Quantcast
Channel: MAFUNDISHO – Strictly Gospel
Viewing all articles
Browse latest Browse all 46

Tugeuzwe nia Zetu!

$
0
0

nia

Kugeuzwa nia ni jambo endelevu na la kujizoeza; lakini haliwezekani bila mhusika kuamua kwa dhati. Ni jambo linalotaka maamuzi sahihi na thabiti. Kugeuzwa nia; A) ni utakaso wa mwili mbali na uchafu (makosa, hila, ila, maovu) na tamaa mbaya zote, B) ni kutakaswa mawazo na utu/nia wa/ya ndani ili kuwa na dhamiri njema siku zote mbele za Mungu na wanadamu  C) ni kujidhiri ili Mungu akukweze, (fanya yaliyo kinyume na elimu na uchumi wako kwa ajili ya Kristo) D) ni kutengeneza njia na kauli zako ili uyale mema ambayo ni tunda la ulimi wako, E) ni kumwamini Mungu pacpo mashaka wala hofu hata km akili/hali/mazingira havikubali. F) ni kujisimamia na kukisimamia kile ulichoamini na kuendelea kukiri moyoni na hadharani pacpo mashaka maana hofu na mashaka vina adhabu na kutokumwamini Mungu kuna adhabu pia tena kubwa.

Kwa ujumla kugeuzwa upya nia ya roho sio njia rahisi, ina maumivu na mateso. Lakini kwa kuwa aliyetuita hakutuitia raha za dunia ambazo ni za muda mfupi bali za milele ambazo zimehifadhiwa juu ambako nondo wala kutu havigusi, na wala hakusema kuwa hatutateswa ni vema kuamua kumfuata ipasavyo. Nia ya roho ya mtu isipogeuzwa, wokovu wake ni sawa na ubatili na kujilisha upepo. kwanini? jibu lake ni rahisi…“itakufaa nini kuupata ulimwengu wote na kupoteza nafsi yako milele? Kumpokea Yesu ni hiari (mtu halazimishwi) lakini ukishakuwa wake huna hiyari tena ila kufuata nyayo zake kikamilifu. Iko NEEMA ya kukuwezesha, haiji yenyewe bali yampasa mtu kukiendea kiti cha rehema cha Kristo ili akupe NEEMA hiyo. Geuzwa Nia!

Mtu asipogeuzwa nia ya roho yake ni hakika kuyatenda mapenzi ya Mungu kwa mtu huyu ni ngumu sababu dunia na mambo yake na tamaa zake vinaimba wimbo wa kutoitii sheria ya Mungu ndani ya mtu huyu bila kutaka atautii wimbo huo, kwa hiyo si rahisi kuwatumikia mabwana wawili. Lazima mtu huyu ataambatana zaidi na yule anayemuona (dunia, anasa, tamaa ya mali na mwili, kiburi cha uzima, majivuno, dharau, masengenyo, masimango, wivu, husuda, mizaha, kejeri, uzinifu na uasherati, uongo, uchoyo, uuaji wa mwili na roho, mawazo na nia mbaya, unafiki, kutosamehe, kutoachilia, uchungu, hila na ndugu zao) kuliko Yesu ambaye anaonekana kwa Imani.

Namshauri kila mmoja wetu, pamoja na u-busy ulio nao, popote ulipo na kila ufanyalo,
jizoeshe kumwambia Mungu hivi;
1. UKINIGEUZA NITAGEUKA. (na ndani yako iwepo nia ya kugeuka ugeuzwapo/ukunjwapo na Neno)
2.NIVUTE KWAKO NIWE WAKO MILELE(sababu dunia nayo inavuta sana kuelekea kwake so lazima ukubali kumilikiwa na BWANA Yesu)
3. NICHUNGUZE EE BWANA NA UNITAKASE MOYO, MWILI NA NAFSI YANGU.
4. NILINDE NA NJIA MBAYA NA NIEPUSHE NA MARAFIKI WAOVU KWA GHARAMA  YOYOTE
( na uwe tayari hayo yanapokujia kwani maranyingi hatuko tayari kutengwa na rafiki zetu ht km ni waovu so stm Mungu hutumia vituko km dhuluma, magomvi etc kututenga nao) Maombi haya ni ya kila mtu lakini yana matokeo ya wazi kwa mtu aliyeamua kugeuzwa nia ya roho yake kwa kumaanisha.

Kwa jinsi hii, kuna kila sababu ya kukubali binafsi kugeuzwa roho za nia zetu ili tuvikwe utu mpya na kwa ujumla wake ni kujifunza kwa bidii na gharama kubwa (km Yesu wetu) kuwa WANYENYEKEVU na WATIIFU bila kujali gharama hizo.
 

NAWAPENDA KWA KUWA KRISTO ALIAGIZA UPENDO.

Gladys!


Filed under: MAFUNDISHO

Viewing all articles
Browse latest Browse all 46

Trending Articles